Polisi Uganda wazingira nyumba ya Besigye

Kiongozi wa upinzani Uganda Dr. Kizza Besigye.

Polisi Uganda wazingira nyumba ya kiongozi wa upinzani Dr. Kizza Besigye

Polisi nchini Uganda wamezingira nyumba ya kiongozi wa upinzani Kizza Besigye ambaye aliwahi kukamatwa mara kadhaa mwaka huu kwa kuongoza maandamano dhidi ya ongezeko la bei za bidhaa.

Maafisa wa chama kikuu cha upinzani wamesema polisi walizingira nyumba ya bwana Besigye katika mji wa Kampala leo na kuweka vizuwizi vya barabarani katika eneo hilo. Hakuna maelezo zaidi yaliyotolewa na polisi wa Uganda. Polisi walimkamata Besigye takriban mara nne alipoongoza maandamanao ya “ kutembea kwenda kazini” kupinga ongezeko la bei ya chakula na mafuta mwezi April.