Obama awahimiza wananchi kujihusisha na siasa

Rais Obama akiwapungia wageni alipowasili ukumbi wa McCormick huko Chicago, kutoa hotuba yake ya mwisho kama rais, Jan. 10, 2017.

Rais Barack Obama wa Marekani Jumanne usiku alitoa hotuba yake ya mwisho kwa wananchi wa Marekani, akiwashukuru kumsaidia kukamilisha mipango mingi aliyeahidi kufanya.

Akizungumza katika ukumbi wa McCormick huko Chicago mahala alipoanzia harakati zake za kisiasa akiwa mbele ya maelfu ya watu waliomshangilia huku wakisema “miaka minne zaidi”, Rais Obama aliwahimiza wananchi kuendelea na juhudi za maendeleo na kujiendeleza wenyewe.

Your browser doesn’t support HTML5

Mahojiano ya VOA na Profesa Patrick Nigula wa South Carolina, Marekani

Rais Obama alisema watu wa Marekani wamemfanya awe rais bora na aliwakumbusha kwamba mfumo wa nchi ya Marekani uliokuwepo ni kuwalinda watu wote na sio watu kadhaa.