Mmarekani kutumikia zaidi ya miaka 22 gerezani kwa kusaidia ugaidi

Jaji mmoja wa mahakama kuu ya serikali ya Rochester huko New York alimhukumu Mufid Elfgeeh hiyo jana Alhamisi.

Raia mmoja wa Marekani atatumikia hadi kifungo cha miaka 22 na nusu gerezani kwa kujaribu kutoa mafunzo kwa wapiganaji wa ugaidi na kuchangisha fedha kwa ajili ya kundi la Islamic State.

Jaji mmoja wa mahakama kuu ya serikali ya Rochester huko New York alimhukumu Mufid Elfgeeh hiyo jana Alhamisi.

Waendesha mashtaka wanasema Elfgeeh ni mmoja wa watoaji mafunzo wa kundi la Islamic State ambaye hakuwahi kukamatwa. Alikamatwa akijaribu kuwasaidia wapelelezi wawili wa FBI kwenda Syria mwaka 2014 kujiunga na kundi la Islamic State.