Muathirika huyo aliyenusurika katika shambulio hilo alisema punde baada ya kuokolewa kuwa “anajisikia vizuri,” baada ya madaktari kumuweka katika kitanda cha wagonjwa na kumbeba mtu huyo aliyeonekana kutodhurika
Makombora ya Russia huko Kharkiv yaliwajeruhi watu zaidi ya 40 wakiwemo watoto, mamlaka zimesema.
Makombora kadhaa yalipiga eneo la maduka na ukumbi wa sherehe majira ya mchana katika mji wa mashariki.
Vikosi vya Ukraine vimeushambulia mkoa wa kusini mwa Russia la mkoa wa Belgorod siku ya Jumapili, na kujeruhi watu 11 wakiwemo watoto wawili ambao wamejeruhiwa vibaya, gavana wa mkoa huo Vyacheslav Gladkov amesema.
Gladkov, aliandika ujumbe kwenye mtandao wa Telegram, alisema wavulana wawili wanafanyiwa upasuaji baada ya kupata majeraha mabaya mmoja wao akiwa na majeraha makubwa kwenye miguu yote miwili. Madaktari wanafikiria kuwapeleka Moscow kwa ajili ya matibabu zaidi.
Shambulio limeharibu nyumba 22 makazi ya watu na nyumba binafsi nane pamoja na magari zaidi ya 20, amesema.
Shrika la habari la Reuters halikuweza kuthibitisha kutoka vyanzo huru juu ya idadi hiyo. Maafisa wa Ukraine hawakutoa maoni.