Mshambuliaji ajiua baada ya kuua watu 3 na kujeruhi 5 Marekani

Polisi wakishika doria baada ya mtu aliyejihami kwa bunduki kuua watu katika chuo kiuu cha Michigan

Mshambuliaji aliyekua na bunduki amejiua baada ya kuwaua watu watatu na kujeruhi wengine watano katika chuo kikuu cha Michigan hapa Marekani.

Mtu huyo mwenye umri wa miaka 43 alijiua baadaeye, alipokumbana na polisi kufuatia msako uliodumu saa kadhaa na polisi wamesema kwamba alikuwa na uhusiano na chuo hicho.

Sababu ya kufanya shambulizi hilo haijulikani.

Maafisa hawajatoa taarifa zaidi kuhusu mtu huyo ikiwemo majina kamili na uhusiano wake na chuo hicho cha jimbo la Michigan