Watu wauwawa katika mapigano mapya Sudani Kusini

Darzeni ya watu wanahofiwa wameuwawa baada ya mapigano kuzuka jana Jumatatu kati ya wanajeshi wa Serikali ya Sudan Kusini na kundi lisilojulikana na wapiganaji katika mji wa Raja uliyoko katika jimbo la Lol.

Kiongozi mmoja wa kanisa amesema zaidi ya wakazi 400 wamekimbia na kutafuata hifadhi katika kanisa la kikatoliki huko Raja.

Vyanzo mjini Raja vinaeleza kwamba Gavana wa jimbo hilo, Rizik Zacharian Hassan, na maafisa wengine wa jimbo wemkekimbia kutoka jimbo hilo.