Wanasiasa wajianda kwa uchaguzi mdogo Kenya.

Nairobi Kenya.

Nchini Kenya wakati huu, vyama vya upinzani vimejipata tena kwenye mizani ya uongozi wakati ikiwa imebakia chini ya kipindi cha miaka miwili kabla ya uchaguzi mkuu kufanyika nchini humo.

Your browser doesn’t support HTML5

Kampeni Kenya.

Viongozi wa vyama vya upinzani na hasa chama CORD,pamoja na wale wa muungano wa Jubilee uliounda Serikali wamejipata kwenye joto la kisiasa na malumbano makali kwenye kampeni za uchaguzi mdogo uinazotarajiwa kufanyika katika kipindi cha wiki mbili.

Uchaguzi huo ni za kuwachagua wabunge wapya na Seneta mmoja baada ya nafasi zao kutangazwa wazi na Tume huru ya Uchaguzi na Mipaka ya Kenya. Tume hiyo imekuwa ikilaumiwa na dbaadhi ya viongozi kwa kuzembea kwenye shughuli ya uandikishaji wa wapiga kura wapya, lakini inasema kuwa mikakati ya uandukishaji imebadilika.