Majina ya waathirika wa shambulizi la kigaidi la Somalia kutolewa baada ya familia zao kujulishwa.

Wanajeshi wa Kenya wakiwa kwenye sherehe katika picha ya awali.

Idara ya Ulinzi ya Kenya imesema haiwezi kutangaza hadharani idadi ya wanajeshi waliouawa nchini Somalia mapema Ijumaa iliopita,kabla ya kufahamisha familia zao.

Your browser doesn’t support HTML5

Wanajeshi wa Kenya.


Wakati huo huo mamlaka ya inaendelea kufuatilia kwa makini watu wanaodaiwa kusambaza picha kupitia mitandao ya kijamii,zinzazoonyesha wanajeshi wengi wakiwa wameuwawa na wanamgambo wa Al Shabaab.

Mkuu wa jeshi la Kenya la KDF, Samson Mwathethe amesema kuwa shambulizi hilo lilisababisha maafa wa wanajeshi wa muungano na vile vile wanamgambo wa Al shabab.