Baraza la Seneti : Matukio muhimu ya kesi inayoendelea dhidi ya Rais Donald Trump

Baraza la Seneti la Bunge la Marekani laanza kusikiliza hoja za awali juu ya kesi ya inayotaka kumuondoa Rais Donald Trump madarakani, Jumatano, Januari 22, 2020.

Karani wa Bunge Cheryl Johnson akishikilia nyaraka za mashtaka dhidi ya Rais Donald Trump kwa ajili ya kuzikabidhi katika Baraza la Seneti ndani ya Bunge la Marekani, Washington.

Kiongozi mwendesha mashtaka wa Kamati ya Usalama Mwenyekiti Adam Schiff wa Chama cha Demokrat akiongea katika ufunguzi wa mjadala katika kesi ya kumuondoa madarakani Rais Donald Trump inasikilizwa katika Baraza la Seneti.

Afisa muungozaji kesi Jaji Mkuu John Roberts akiwaapisha wajumbe wa Baraza la Seneti kuendesha mashtaka dhidi ya Rais Donald Trump ndani ya Bunge la Marekani, mjini Washington, Alhamisi, Jan. 16, 2020. (Senate Television via AP)

 Kiongozi wa waliowengi katika Baraza la Seneti Mitch Mc Connell, kulia, akiwa na Katibu wa waliowengi Laura Dove, kushoto, akirejea katika ukumbi wa Bunge mjini Washington, Jumanne usiku, Januari 21, 2020.(AP Photo/J. Scott Applewhite)

Jaji Robert Johnson akiongea wakati wa kuanza kwa kesi ya kumuondoa madarakani Rais Donald Trump.

Usiku wa Jumanne, Januari 21, 2020, ambapo kesi dhidi ya Rais Donald Trump iliendelea kusikilizwa hadi usiku wa manane.

Maseneta wakipiga kura kuwasilisha marekebisho yaliyoletwa na Kiongozi wa Wademokrat waliowachache katika Baraza la Seneti Chuck Schumer, katika Ukumbi wa Bunge la Marekani, Jumatano, Jan. 22, 2020. (Senate Television via AP)

Kiongozi wa waliowachache katika Baraza la Seneti Chuck Schumer akizungumza na waandishi wa habari kabla ya kesi dhidi ya Rais Donald Trump kuanza

Baraza la Seneti la Bunge la Marekani laanza kusikiliza hoja za awali juu ya kesi inayotaka kumuondoa Rais Donald Trump madarakani, Jumatano, Januari 22, 2020.