Ajali yaua 5, kujeruhi 7 Kenya

Watu watano wakiwemo watoto wawili wamefariki, huku wengine zaidi ya saba kujeruhiwa vibaya katika ajali ya basi nchini Kenya

Ajali hiyo imetokea Jumanne huko eneo la Ndara, Voi katika barabara kuu ya Mombasa-Nairobi.

Gari aina ya matatu iligongana na lori katika eneo la Ndara wakati ikijaribu kupita gari jingine kabla ya kugongana uso kwa uso na lori.