Ghasia za kidini zaibuka tena Nigeria

Watu 13 wameuwawa katika ghasia nyingine za kidini na kikabila zilizotokea Nigeria ya kati.

Maafisa wanasema wafugaji wa kiislam walivamia kijiji cha wakristo kusini mwa mji wa Jos mapema leo wakichoma nyumba na kushambulia watu kwa mapanga huku wakikimbia nje.

Mashahidi wanasema washambuliaji hao walivalia sare za kijeshi.

Mji wa Jos na vitongoji vyake una historia ya ghasia za kidiini ikiwa inachochewa kwa kiasi fulani na ushindani wa udhibiti wa maeneo yenye rutuba.