Siku 100 za Urais wa Obama

Wachambuzi wengi wa siasa na wanauchumi wamepongeza mafanikio yaliyofikiwa na hatua alizochukua kukabiliana na migogoro kadhaa inayoikabili Marekani.

Wanasema katika kipindi hicho, Bwana Obama ameweza kushughulikia ipasavyo mgogoro wa uchumi Marekani na duniani, mwelekeo wa Marekani katika vita yake nchini Iraq na Afghanistan, kubadili sera za Marekani katika kukabiliana na wafungwa kutoka maeneo ya vita, na juhudi zake za kuboresha uhusiano wa Marekani na mataifa mengine duniani.

Akisukumwa na ujumbe wa mabadiliko, Bwana Obama alibadili baadhi ya sera zilizokuwa zimewekwa na mtangulizi wake, George W. Bush, hatua ambayo aliweza kui