Papa Francis akamilisha ziara yake ya Sudan Kusini na DRC

Papa Francis yuko ndani ya ndege akirudi Vatican baada ya ziara ya siku sita nchini Sudan Kusini na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo

Papa Francis (kati kati) aongoza Misa Takatifu siku ya Jumapili, kwenye uwanja wa makumbusho wa John Garang siku ya mwisho ya ziara yake Sudan Kusini 

Papa Francis akimuombea Rais Salva kiir wa Sudan Kusini wakati wa sherehe za kumuaga kabla ya kuondoka Juba, Sudan Kuisni 

Waumini wa Sudan Kusini wakihudhuria Misa inayoongozwa na Papa Francis mjini Juba, Jumapili Feb 5, 2023.

Wananchi wa Sudan Kusini wasikiliza hotuba ya Papa Francis wakati wa Misa Takatifu mjini Juba.

Papa Francis akiwapungia mkono waumini alipokua anazunguka ndani ya gari lake kwenye uwanja wa John Garan mjini Juba. 

Makasisi na Watawa wahudhuria Misa Takatifu inayoongozwa na Papa Francis. 

Waumini wanaimba Kwaya wakati Papa Francis akiongoza Misa mjini Juba.

Papa Francis amekamilisha ziara yake ya siku 6 nchini Sudan Kusini na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, kwa Misa Takatifu kwenye uwanja wa makumbusho wa John Garang, mjini Juba, siku ya Jumapili.