Ahadi ya Marekani yaipa imani Korea Kusini

Waziri wa Ulinzi wa Korea Kusini Lee Jong-sup akizungumza alipohudhuria mkutano na waandishi wa habari pamoja na Waziri wa Ulinzi wa Marekani Lloyd Austin baada ya mkutano wao katika Wizara ya Ulinzi huko Seoul, Korea Kusini, 31 Januari 2023. REUTERS.

Mjumbe wa ngazi ya juu wa nyuklia wa Korea Kusini alisema makubaliano na Marekani ya kuimarisha kwa pamoja uzuiaji wa muda mrefu dhidi ya Korea Kaskazini unaipa utawala wa Yoon imani inayohitajika kuwa muungano huo utaweza kujilinda vilivyo dhidi ya uchokozi kutoka Pyongyang.

Ahadi ya Marekani, iliyoainishwa katika taarifa ya pamoja ya nchi hizo mbili katikati ya mwezi wa Septemba, inajumuisha uthibitisho kwamba jaribio la nyuklia la Korea Kaskazini litakabiliwa na jibu kubwa na thabiti.

Inaongeza kuwa nchi hizo mbili zitaendelea na kuimarisha mashauriano ya karibu ya Muungano kuhusu sera ya Marekani ya ulinzi wa nyuklia na makombora.