Rais Kabila Afanya Ziara Mji wa Vita

Rais Joseph Kabila wa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) amefanya ziara ya kutembelea mji wa Oicha, uliopo Beni, kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.

Kwa mujibu wa muandishi wa habari Austere Malivika aliyeshuhudia ziara ya Rais Kabila amesema kiongozi huyo ameahidi kupatikana kwa amani katika eneo hilo kwa haraka.

Ziara ya Rais Kabila ya Oicha imekuja wakati eneo hilo likiwa linakumbwa na mapigano yanayofanywa na vikundi vya uasi nchini DRC.

Vikundi ambavyo vinadaiwa kuvuruga amani ya eneo hilo inasemekana vinatoka nchini Uganda pamoja na raia wa nchi nyingine.

Unaweza kusikiliza taarifa ya mwandishi wetu Austere Malivika wa DRC.

Your browser doesn’t support HTML5

Ripoti ya Austere Malivika kuhusu ziara ya Rais Joseph Kabila