Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Januari 22, 2025 Local time: 00:53

Watu 11 wamefariki na wengine kujeruhiwa kufuatia ajali ya moto Ufaransa


Wafanyakazi wa zimamoto wakiwa kwenye tukio katika eneo la Wintzenheim huko France. Aug. 9, 2023.
Wafanyakazi wa zimamoto wakiwa kwenye tukio katika eneo la Wintzenheim huko France. Aug. 9, 2023.

Moto huo ulizuka Jumatano asubuhi katika mji wa Wintzenheim. Maafisa  wanasema nyumba hiyo ilikodishwa na chama ambacho  kinawasaidia watu wenye ulemavu. Wakazi hao ambao hawajulikani waliko wakiwemo watu wazima 10 wenye ulemavu na mfanyakazi mmoja walikuwa  wanatokea mji wa mashariki wa Nancy.

Maafisa wa zima moto wanasema miili tisa imepatikana kutoka kwenye vifusi vya moto mkubwa katika jengo linalotumika wakati wa likizo huko mashariki mwa Ufaransa ambapo watu 11 waliripotiwa kupotea.

Moto huo ulizuka Jumatano asubuhi katika mji wa Wintzenheim. Maafisa wanasema nyumba hiyo ilikodishwa na chama ambacho kinawasaidia watu wenye ulemavu. Wakazi hao ambao hawajulikani waliko wakiwemo watu wazima 10 wenye ulemavu na mfanyakazi mmoja walikuwa wanatokea mji wa mashariki wa Nancy.

Christopher Marot, kiongozi wa wilaya ya Haut-Rhin aliwaambia waandishi wa habari mapema Jumatano kwamba hakuna ishara kwamba watu 11 waliopotea, walifanikiwa kukimbia moto huo. Moto huo ulidhibitiwa haraka, lakini Waziri wa Mambo ya Ndani Gerald Darmanin aliandika kwenye mtandao wa kijamii wa X, ambao zamani ulijulikana kama Twitter kwamba vifo kadhaa vimeripotiwa kutoka eneo la tukio na kwamba shughuli za uokoaji bado zinaendelea.

Watu wengine 17 waliokolewa kutoka kwenye moto huo, huku mtu mmoja akisafirishwa hadi hospitali iliyo karibu. Waziri Mkuu wa Ufaransa, Elisabeth Borne amesema kupitia mtandao wa X kwamba anaelekea eneo la tukio hilo. Sala yangu ya kwanza ni kwa waathirika na wapendwa wao, aliandika.

Forum

XS
SM
MD
LG