Zikiwa zimesalia siku chache kwa Wazanzibari na Watanzania kwa ujumla kupiga kura katika uchaguzi mkuu, baadhi ya wapiga kura wa Zanzibar bado hawajawa na uhakika kamili wa ushiriki wao katika uchaguzi wa Jumapili.
Wakizungumza katika ofisi ya tume ya chaguzi Zanzibar wengi wao wamelalamikia kuhusu kutokuwa na vitambulisho vya kupigia kura ambapo siku ya mwisho ya kuvipata ilikuwa Octoba 20 .
Suala hilo limeleta hisia tofauti kwa wapiga kura ambao kama hawataruhusiwa kutekeleza zoezi hilo basi watakuwa wamekosa haki yao ya msingi.