Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Aprili 20, 2024 Local time: 11:06
VOA Direct Packages

Wanaharakati wa Zimbabwe wadai ZANU-PF kimeingilia simu za wapiga kura


Bango nje ya ofisi za tume ya kitaifa ya uchaguzi ya Zimbabwe, ZEC
Bango nje ya ofisi za tume ya kitaifa ya uchaguzi ya Zimbabwe, ZEC

Wanaharakati wa haki za kijamii nchini Zimbabwe Jumanne wamesema kwamba watachukua hatua za kisheria baada ya madai kwamba baadhi za simu za wapiga kura ziliingiliwa na kutumiwa ujumbe unaounga mkono chama tawala cha ZANU-PF.

Zimbabwe inaelekea kwenye uchaguzi mkuu baadaye mwaka huu ukitarajiwa kuwa wenye ushindani mkubwa, wakati chama ZANU-PF tayari kikilaumiwa kuzima sauti za upinzani. Kwa mujibu wa shirika la habari la AFP, baadhi ya wapiga kura katika siku 5 zilizopita wamedai kupojea ujumbe unaoisifu serikali kwenye simu zao za mkononi.

Ujumbe wanaopokea unasemekana kuandikwa kwa lugha ya kishona, ukijumuisha jina la mwenye simu, wilaya yake na kutiwa saini ya “ Rais ED Mnangagwa”. Kundi la wanaharakati la Team Pachedu, linailaumu tume ya uchaguzi ya Zimbabwe ZEC, kwa kutoa taarifa za wapiga kura kwa chama tawala cha ZANU-PF, ukiwa ukiukwaji mkubwa wa usiri wa watu pamoja na sheria za uchaguzi.

XS
SM
MD
LG