Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 28, 2024 Local time: 20:19

Viongozi wa Afrika watoa wito kwa wapiganaji wa M23 kuondoka Goma


Wacongo wakimbia vita kutoka mji wa Sake, 27km magharibi ya Goma, Nov. 23 2012.
Wacongo wakimbia vita kutoka mji wa Sake, 27km magharibi ya Goma, Nov. 23 2012.
Viongozi wa mataifa ya Afrika Mashariki na Kati walikutana Jumamosi mjini Kampala kujaribu kutanzua mzozo unaoendelea mashariki ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Mkutano huo ulohudhuriwa na Marais wa Uganda, Tanzania Kenya na Congo ulipendekeza mpango wenye nukta nane, juu ya jinsi ya kutanzua mzozo huo.

Rais Paul Kagame ambae anatuhumiwa na ripoti ya Umoja wa Mataifa kwamba anawafadhili wapiganaji wa M23 hakuhudhuria mkutano na katika dakika za mwisho alimtuma waziri wake wa mambo ya nchi za nje, Bibi. Louise Mushikiwabo.

Viongozi hao wamewataka pia waasi wa kundi la M23 kusitisha mara moja mashambulizi yao na kuondoka Goma. Wamependekeza pia kuwepo na kikosi cha kimataifa kwenye uwanja wa ndege wa Goma ikiwahusisha majeshi ya Tanzania na DRC

Umoja wa mataifa imeituhumu Rwanda kwa kuwasaidia waasi hao wa M23, jambo Kigali inakanusha. Mkutano huo wa viongozi mjini kampala umefanyika kukiwa na wasi wasi kwamba waasi wanasonga mbele huko mashariki ya nchi na kukiwepo na mabadiliko katika jeshi la Congo.

Kwa upande mwengine mashirika ya misaada ya dharura yanaeleza wasi wasi wao kutokana na ukatili unaotendewa raia ambao wengi wako njiani wakikim bia vita. Kuna ripoti za maiti kuonekana njiani kati ya Goma kuelekea upande wa kusini.
XS
SM
MD
LG