Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 23:50

Mfumo mpya wa utawala Kenya unaanza kwa msukosuko


Mwaziri 15 wa baraza jipya la serikali ya Kenya walianza rasmi kazi Alhamisi, baada ya kuapishwa na Rais Uhuru Kenyatta siku ya Jumatano. Bunge kwa wingi mkubwa liliidhinisha Jumanne majina ya mawaziri wote 16 waloteuliwa na Rais Kenyatta.

Wachambuzi na Wakenya wengi wameeleza kuridhika na mawaziri waloteuliwa na kuwatakia kazi njema, wakti huo huo kusifu utaratibu mpya wa kuwachunguza kwanza bungeni kabla ya kuapishwa.

Huku serikali mpya ikichukua madaraka, hali ya wasi wasi inaendelea katika serikali za wilaya zinazojulikana kama County, kutokana na matatizo kadhaa ya uchukuzi, mahali ya kufanya kazi na wabunge wa mabaraza ya County wanagoma wakidai mishahara zaidi.
"Live Talk"- Mfumo mpya wa utawala Kenya - 17:28
please wait

No media source currently available

0:00 0:17:27 0:00
Kiungo cha moja kwa moja

Katika mjadala wa wiki wa Sauti ya Amerika "Live talk", Seneta Kipchumba Murkomen wa County ya Ilgio Marakwet, anasema ni mapema kukosowa utaratibu mpya wa utawala, kwani kila kitu kipya hakikosi mashaka. Anasema inabidi kuwapati viongozi wepya nafasi kuanza kazi ndipo watu waweze kukosowa baadae.

Mwanaharakati Afiya Rama wa Mombasa anasema utawala umeanza na misukosuko mingi na inatia wasi wasi kwani kutokana na ukosefu wa uwongozi thabiti kwa hivi sasa uhalifu uemezidi kote nchini, hata hivyo inabidi kuwa watulivu na kuwapatia viongozi wepya nafasi ya kufanya kazi.

Mbunge wa Kwamaiko County karibu na Nairobi Karungo wa Thangwa katika "LIve Talk anasema ameweka ofisi yake kwenye soko ili kuweza kuwasiliana na walomchagua na kumulika tatizo kubwa na watu kutokuwa tayari kwa mfumo mpya na wawakilishi wengi hawana hata mahali ya kufanya kazi.
XS
SM
MD
LG