Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Oktoba 02, 2023 Local time: 20:38
VOA Direct Packages

Ufaransa yakabiliana na mzozo wa kidiplomasia kufuatia matamshi ya Macron dhidi ya Marekani


Rais wa Marekani Joe Biden na mwenzake wa Ufaransa Emmanuel Macron.

Ufaransa inajaribu kuzuia mzozo wa kidiplomasia kufuatia matamshi ya rais Emmanuel Macron kwamba Ulaya inahitaji kupunguza utegemezi wake wa Marekani, na kuepuka kujikuta  katika  migogoro isiyo wahusu, wakati akiwa kwenye ziara rasmi nchini China mapema mwezi huu.

Wakosoaji wake wanasema kwamba matamshi hayo yanahujumu ushirikiano wa mataifa ya Atlantic, wakati ulimwengu ukishuhudia taharuki za kisiasa za kieneo. Macron aliitembelea Beijing Aprili 5-8 akiandamana na mkuu wa EU, Ursula von der Leyen, kwa sehemu moja kuisihi china kusaidia katika kumaliza uvamizi wa Russia wa Ukraine.

Miongoni mwa watu wangine walioandamana na viongozi hao ni wafanyabiashara mashuhuri kutoka Ulaya, na ambao walitia saini mikataba kadhaa ya kibiashara. Kufikia sasa, China haijakemea uvamizi wa Russia wa Ukraine ulioanza Februari mwaka jana, na rais Xi Jinping pia alijiepusha kuzungumzia hilo wakati wa ziara ya Macron.

XS
SM
MD
LG