Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 11:16
VOA Direct Packages

Tunisia yamfukuza afisa wa chama cha wafanyakazi wa Ulaya


Baadhi ya wafanyakazi walioshiriki kwenye maandamano ya Tunisia.
Baadhi ya wafanyakazi walioshiriki kwenye maandamano ya Tunisia.

Rais wa Tunisia Kais Saied ameamuru afisa wa ngazi ya juu wa chama cha wafanyakazi cha Ulaya kuondoka nchini baada ya kuhutubia watu waliokusanyika kwenye maandamano yalioitishwa na umoja wa vyama vya wafanyakazi  nchini humo.

Kwa mujibu wa shirika la habari la AP, serikali inalaumu Esther Lynch ambaye ni katibu mkuu wa muungano wa vyama vya wafanyakazi vya Ulaya kutoka Ireland kwamba ameingilia masuala ya ndani ya Tunisia wakati wa maandamano ya Jumamosi kwenye mji wa Sfax, yakilalamikia utawala wa Saied.

Muungano wa vyama vya wafanyakazi nchini humo UGTT, uliitisha maandamano ya kitaifa kupinga msako unaofanywa na serikali dhidi ya wapinzani wa kisiasa, wanahabari, majaji, wafanyabiashara pamoja na viongozi wa vyama vya wafanyakazi.

Wakati akihutubia waandamanaji. Lynch aliitisha kuachiliwa kwa kiongozi wa wafanyakazi Anis Kaabi aliyekamatwa na maafisa wa usalama mwezi uliopita. Aliomba serikali kushauriana na uongozi wa UGGT, pamoja na kuimarisha uchumi ambao unaelekeza taifa hilo kufilisika. Mzozo wa kisiasa umeendelea kuongezeka baada ya uchaguzi wa bunge mwezi uliopita, uliovutia asilimia 11 pekee ya walipigakura.

XS
SM
MD
LG