Tume huru ya uchaguzi nchini Ghana imekanusha haraka shutuma za kufanya uamuzi wa kuwazuiya wagombea kushiriki kwenye uchaguzi mkuu wa Desemba 7 kwa sababu ya kutokidhi viwango , kwamba ulikuwa na ushawishi wa kisiasa.
Tume hiyo iliwazuiya wagombea 12 ikiwemo mke wa zamani wa rais, Nana Konadu Agyemand Rawlings mgombea urais kupitia chama cha national democratic party, kwa kushindwa kufikia masharti ya uteuzi yaliyotakiwa kuwakilishwa kabla ya November 30.
Tume ya uchaguzi imesema wagombea walio na viwango vya kushiriki katika uchaguzi mkuu ni pamoja na rais aliyoko madarakani John Dramani mahama .
Katika mahojiano na sauti ya amerika msemaji wa tume ya uchaguzi Eric Dzakpasu amesema tume hiyo inafanya kazi kwa kufuata sheria za uchaguzi.
Facebook Forum