Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Aprili 23, 2024 Local time: 17:08

Takriban watu kumi wauwawa katikati mwa Syria mwishoni mwa wiki


Mabaki ya gari lililopigwa bomu nchini Syria kwenye picha ya maktaba. Oktoba 11, 2021.
Mabaki ya gari lililopigwa bomu nchini Syria kwenye picha ya maktaba. Oktoba 11, 2021.

Takriban watu 11 wengi wao raia wameuwawa katikati mwa Syria kwenye shambulizi linaloshukiwa kutekelezwa na kundi la kigaidi la Islamic State.

Kundi la kutetea haki za binadamu la Syrian Observatory for Human Rights limesema kwamba takriban watu 75 walishambuliwa na kundi hilo Jumamosi kwenye eneo la mashambani la Homs mashariki mwa taifa hilo.

Watu 10 waliuwawa akiwemo mwanamke mmoja, pamoja na mpiganaji kutoka vikosi vya utawala wa Syria, huku baadhi ya watu wakiwa hawajulikani walipo, ripoti ya kundi hilo imeongeza.

Shirika la habari la serikali ya Syria la SANA limeripoti kuhusu shambulizi hilo ingawa limetoa idadi ndogo ya waliokufa ikilinganishwa na ripoti ya awali.

Ghasia za Syria zilizoanzishwa na harakati za kukomesha maandamano ya kudai demokrasia miaka kadhaa iliyopita, zimeua takriban watu nusu milioni kufikia sasa, huku takriban nusu ya wakazi wa taifa hilo wakilazimika kuondoka makwao.

XS
SM
MD
LG