Cristiano Ronaldo na Al Nassr waltupwa nje ya Saudi Super Cup baada ya kuchapwa mabao 3-1 na Al Ittihad siku ya Alhamisi.
Nyota huyo wa Ureno hajawa na mwanzo mzuri katika klabu yake mpya ya Al Nassr ya nchini Saudi Arabia, kwani alishindwa kufunga bao kwenye mechi ya pili mfululizo.
Katika mechi yake ya kwanza kwa timu yake ya Al Nassr dhidi ya Ettifaq, Ronaldo hakuwa na hata na shuti moja lililolenga lango.
Katika mechi iliyofuata Al Nassr walifanikiwa kupata ushindi dhidi ya timu ya Al Fateh siku ya Ijumaa kwa jumla ya mabao 2-1.
Facebook Forum