Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Julai 26, 2026 Local time: 12:00

Raia 34 na wanajeshi sita wamefariki katika shambulio nchini Burkina Faso

Wanajeshi wa Burkina Faso wakifanya doria katika baadhi ya maeneo nchini humo
Wanajeshi wa Burkina Faso wakifanya doria katika baadhi ya maeneo nchini humo

Kikosi cha wanajeshi na raia wa kujitolea walilengwa katika shambulio la watu wasiojulikana wenye silaha karibu na kijiji cha Aorema kilichoko kaskazini ya Burkina Faso gavana wa eneo hilo alisema katika taarifa

Takriban raia 34 wa kujitolea na wanajeshi sita walifariki katika shambulio linaloshukiwa kufanywa na wanajihadi huko kaskazini mwa Burkina Faso serikali ya mtaa katika eneo hilo ilisema Jumapili.

Kikosi cha wanajeshi na raia wa kujitolea walilengwa katika shambulio la watu wasiojulikana wenye silaha Jumamosi, muda wa saa kumi jioni kwa saa za huko karibu na kijiji cha Aorema gavana wa eneo hilo alisema katika taarifa akiongeza kuwa idadi ya awali ya vifo ilikuwa wasaidizi wa kujitolea 34 na wanajeshi sita.

This item is part of
XS
SM
MD
LG