Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Julai 27, 2024 Local time: 04:17

Paris St Germain na Bayern Munich wanakutana katika UEFA Champions League hatua ya 16 bora


Mshambuliaji wa Paris St Germain Neymar Jr akijishika kiuno baada ya Ruslan Malinovskyi wa Olympique de Marseille kufunga bao la pili katika mchezo wao wa Februari 8,2023 REUTERS
Mshambuliaji wa Paris St Germain Neymar Jr akijishika kiuno baada ya Ruslan Malinovskyi wa Olympique de Marseille kufunga bao la pili katika mchezo wao wa Februari 8,2023 REUTERS

Timu ya Paris St, Germain na Bayern Munich wanakutana katika UEFA Champions League hatua ya 16 mkondo wa kwanza Jumanne 14 Februari.

Bayern na PSG wanapata shida kukwepana hivi karibuni wamekutana katika kampeni zao nne kati ya sita zilizopita, haswa wakati Bayern au Bavarians walipoifunga PSG katika fainali ya Ligi ya Mabingwa 2020.

Kikosi cha Julian Nagelsmann -Bayern kilishinda mechi zote sita za hatua ya makundi, lakini Paris walipita bila kushindwa pia. Ilikuwa ni magoli yalioweka tofauti kati ya timu hizi zilipokutana mara ya mwisho, katika robo fainali ya 2020/21, na pambano lingine hivi karibuni haliepukiki.

Katika mtanange mwingine Totenham Hotspur itakwaana na AC Milan kwenye uwanja wa Giussepe Meaza mjini Milan.

XS
SM
MD
LG