Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Aprili 21, 2025 Local time: 21:32

Netanyahu na Erdogan wafanya kikao nadra cha moja kwa moja mjini New York


Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu, (Kushoto) akisalimia rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan mjini New York, pembeni mwa mkutano wa 78 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.
Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu, (Kushoto) akisalimia rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan mjini New York, pembeni mwa mkutano wa 78 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan na Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu wamekutana Alhamisi  pembeni mwa mkutano wa baraza kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York na kuongeza matumaini ya maridhiano kati ya mataifa yote mawili .

Viongozi hao wamekutana kwa mara ya kwanza moja kwa moja, ikionekana kuwa hatua kubwa kwenye juhudi za karibuni za maridhiano, baada ya kudorora kwa mahusiano hapo nyuma, ambapo wote wawili walirushiana maneno makali.

Kupitia ujumbe wa X iliyojulikana awali kama Twitter, maafisa wa Uturuki wametaja hatua hiyo kuwa muhimu, wakati mazungumzo yakiangazia suala la nishati. Ankara inakaribia Israel kama njia rashisi ya kusambaza gesi kutoka kwenye hifadhi zake nyingi, kuelekea Ulaya.

Waangalizi wanasema kwamba kuendelea kwa ushawishi wa kieneo wa Iran ni suala la kutia wasi wasi. Kuungwa mkono kwa Azerbaijan na wote Israel na Uturuki kunazua wasi wasi kuhusu Tehran, kwa kuwa inaunga mkono hasimu wa Azerbaijan, Armenia.

Ripoti zinasema kwamba Netanyahu na Edorgan wameahidiana kutembeleana hivi karibuni. Ripoti zinaongeza kusema kwamba Edorgan ambaye ni Muislamu, ameelezea azma yake ya kutembelea Jerusalem mwaka huu, na kusali kwenye msikiti wa al Aqsa ambao ni wa tatu kwa utakatifu kwenye dini ya Kiislamu.

Forum

XS
SM
MD
LG