Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Aprili 23, 2024 Local time: 09:44

Mdahalo wa pili wa urais wamalizika Marekani


Rais Barack Obama (R) na mpinzani wake Mitt Romney (L) katika mdahalo wa pili wa urais huko New York, October 16, 2012.
Rais Barack Obama (R) na mpinzani wake Mitt Romney (L) katika mdahalo wa pili wa urais huko New York, October 16, 2012.
Rais Barack Obama wa Marekani amemueleza mpinzani wake Mitt Romney wa chama cha Republican kwamba mpango wake wa kuendeleza punguzo la kodi kwa matajiri utaongeza nakisi na kero kwa wamarekani.

Rais Obama aliyasema hayo wakati wa mdahalo wa pili wa kuwania nafasi ya urais uliofanyika katika mtindo wa wapiga kura kuuliza maswali na kujibu papo kwa papo-ujulikanao kama Town Hall Meeting, kwenye chuo kikuu cha Hofstra huko New York.

please wait

No media source currently available

0:00 0:03:06 0:00
Kiungo cha moja kwa moja

Bwana Romney alimshutumu Rais kwa kutaka kuongeza kodi kwa matajiri. Bwana Romney alisema mpango wake wa kodi utapelekea kuleta ukuaji wa nafasi za ajira na kuwa na bajeti yenye uwiano.

Wagombea hawa wawili walikuwa wakijibu maswali kutoka kwa wapiga kura ambao bado hawajaamua nani wamchague katika uchaguzi mkuu wa nafasi ya urais utakaofanyika Novemba 6.

Sauti ya Amerika-VOA ilifanya mahojiano na mchambuzi wa masuala ya kisiasa bwana Charles Bwenge wa chuo kikuu cha Florida, Marekani na anatoa tathmini yake kuhusu mdahalo huu.
please wait

No media source currently available

0:00 0:02:52 0:00
Kiungo cha moja kwa moja
XS
SM
MD
LG