Umoja wa Afrika unatazamiwa kutuma nchini Burundi wanajeshi 5,000 kutoka kikosi chake cha dharura, kutuliza ghasia zinazoendelea nchini humo.
Serikali ya Uganda ambayo ni mpatanishi mkuu katika maswala ya Burundi imefichua kwamba uamuzi huo umefikiwa kutokana na hali ya kujikokota kuanza mazungumzo ya kumaliza uhasama wa kisiasa nchini humo, huku maafa makubwa yakiendelea kuripotiwa.
Mazungumzo sasa yamepangiwa kuanza tarehe 28 mwezi huu, Mjini Arusha nchini Tanzania.