Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Mei 11, 2024 Local time: 22:42

Mashauriano ya kutafuta amani Ethiopia yatafanyika nchini Tanzania


Waziri Mkuu wa Ethiopia, Abiy Ahmed
Waziri Mkuu wa Ethiopia, Abiy Ahmed

Mashauriano ya Amani ambayo yatafanyika na The Oromo Liberation Army (OLA) yataanza wiki hii nchini Tanzania, Abiy alisema Jumapili. Serikali ya Ethiopia na watu wake watahitaji sana mashauriano haya, aliongeza Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed

Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed anasema serikali yake imeanzisha mazungumzo na kundi la waasi linaloendesha harakati zake katika mkoa wa Oromia, wenye watu wengi na mkubwa sana nchini humo unaozunguka mji mkuu Addis Ababa.

Mashauriano ya Amani ambayo yatafanyika na The Oromo Liberation Army (OLA) yataanza wiki hii nchini Tanzania, Abiy alisema Jumapili. Serikali ya Ethiopia na watu wake watahitaji sana mashauriano haya.

Ninatoa wito kwa kila mmoja kutekeleza jukumu lao. OLA imekuwa ikipambana na serikali kuu ya Ethiopia tangu ilipogawanyika mwaka 2018 na kundi la kihistoria Oromo Liberation Front (OLF) wakati kilipokataa mapambano ya silaha.

Abiy alizungumza kwenye mkusanyiko wa vyama katika mchakato wa Amani wa Tigray ambao ulishuhudia makubaliano hapo Novemba 2 yakimaliza mzozo wa miaka miwili kati ya serikali kuu na kuasi mamlaka za mikoa.

XS
SM
MD
LG