Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 25, 2024 Local time: 13:45

Maelfu ya watu wakusanyika mjini Vatican kwenye mazishi ya Papa Benedict


Malefu ya wa watu waliohudhuria mazishi ya Papa Benedict mjini Vatican, Jan. 5, 2023.
Malefu ya wa watu waliohudhuria mazishi ya Papa Benedict mjini Vatican, Jan. 5, 2023.

Maelfu  ya watu wamekusanyika Alhamisi kwenye bustani ya St Peter mjini  Vatican ili kuhudhuria mazishi ya Papa Emeritus Benedict ambaye aliaga dunia wiki iliyopita akiwa na umri wa miaka 95.

Viongozi mbali mbali kutoka kote ulimwengumi wamekusanyika mjini humo huku maafisa wa usalama wakiwa na kibarua kigumu cha kuhakikisha usalama .

Takriban watu laki moja wanakadiriwa kuhudhuria mazishi hayo kinyume na watu 60,000 kama ilivyokisiwa awali, kulingana na vyombo vya habari vya Italy.

Zaidi ya watu laki mbili wametoa heshima zao za mwisho kwa kiongozi huyo katika siku tatu za maombolezo zilizotengwa za kuutazama mwili wake kwenye kanisa la St Peter’s Basilica.

Ujerumani na Italy ndiyo mataifa pekee yalioalikwa rasmi , wakati viongozi kutoka mataifa mengine wakialikwa kibinafsi.

XS
SM
MD
LG