Ripoti zinasema kwamba ukosefu wa usalama kwenye taifa hilo umefika kwenye viwango vya kutisha. Wakati akiwasilisha hoja yake mbele ya baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, naibu katibu mkuu Amina J. Mohhamed amesema kwamba ingawa kulikuwa na matumaini mwaka mmoja uliopita wa mageuzi ya kisiasa, uthabiti na maendeleo ifikapo mwisho wa mwaka 2022, Haiti imeendelea kugubikwa na kiwango kikubwa cha mzozo usiotarajiwa na kutia wasi wasi mkubwa sana.
Akiripoti kwa baraza hilo kwa njia ya video kutoka Haiti, mkuu wa ofisi ya pamoja ya Umoja wa Mataifa nchini humo Helen la Lime, ametoa takwimu za kutisha kwa kusema kwamba katika mwezi Novemba pekee, mauaji 280 yameripotiwa wakati mengine 1,200 yakiripotiwa mwaka huu, ikiwa idadi ikiongezeka mara mbili ikilinganishwa na mwaka 2021.