Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Aprili 20, 2025 Local time: 09:16

Kimbunga Khanun kurejea tena kwenye kisiwa cha Okinawa, Japan mwishoni mwa wiki


Mti ulioangushwa na kimbunga Okinawa kwenye mji wa Naha Jumatano
Mti ulioangushwa na kimbunga Okinawa kwenye mji wa Naha Jumatano

Kimbuga kilichoharibu nyumba pamoja na mifumo ya umeme kwenye kisiwa cha Okinawa pamoja na vingine nchini Japan, pole pole kimeanza kuelekea magharibi hivi leo, ingawa kinatarajiwa kugeuka na kurejea tena kwenye visiwa hivyo kikiandamana na mvua zaidi.

Kimbunga hicho kilichopewa jina Khanun sasa hivi kipo kwenye maji ya bahari kati ya China na visiwa vya kusini magharibi mwa Japan, kikitarajiwa kusitisha kasi na kisha kugeukia upande wa mashariki kufikia Ijumaa, kulingana na idara ya hali ya hewa ya Japan.

Hadi mvua za centimita 20 zinatarajiwa kwenye eneo la Okinawa kufikia katikati mwa Ijumaa, idara hiyo imeongeza. Kulingana na serikali ya kieneo ya Okinawa, kimbunga hicho kimejeruhi watu 41, watatu miongoni mwao wakijeruhiwa vibaya.

Maelfu ya wakazi wamebaki bila umeme hivi leo kwa kuwa kimbunga hicho kimezuia shuguli za ukarabati kuendelea. Shuguli za usafiri pia zimeathirika ingawa baadhi ya safari za ndege zinatarajiwa kurejea baadaye leo.

Forum

XS
SM
MD
LG