Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Januari 16, 2025 Local time: 09:14

Kampuni ya kusafisha mafuta ya Dangote kuanza shughuli zake Nigeria


Mmiliki ya kiwanda cha kusafishia mafuta cha Dangote cha Nigeria, Aliko Dangote.
Mmiliki ya kiwanda cha kusafishia mafuta cha Dangote cha Nigeria, Aliko Dangote.

Kampuni ya kusafisha mafuta ya Dangote ya Nigeria imeanza kusafisha dizeli pamoja na mafuta ya ndege Jumamosi, baada ya uchelewesho wa  muda mrefu wa ujenzi kwenye kiwanda hicho chenye uwezo wa kuzalisha mapipa 650,000 kila siku.

Kwa mujibu wa shirika la habari la Reuters, kiwanda hicho ndicho kikubwa zaidi barani Afrika, kilichojengwa kwenye peninsula iliyopo nje ya mji mkuu wa kibiashara wa Lagos, kwa gharama ya dola bilioni 20, kikimilikiwa na tajiri mkubwa sana katika bara hilo, Aliko Dangote.

Ingawa Nigeria ndiye mzalishaji wa juu wa mafuta barani Afrika, imekuwa ikitegemea mafuta kutoka mataifa ya nje. Kiwanda cha Dangote sasa kitaiwezesha Nigeria siyo tu kujitegemea, mbali pia kuuza mafuta kwenye mataifa jirani ya Afrika Magharibi, na hatimaye kubadili biashara ya mafuta katika ukanda wa Atlantiki.

Maafisa wa kampuni hiyo wameiambia Reuters kwamba kitaanza majaribio ya wiki hii, baada ya kupokea shehena ya 6 ya mafuta ghafi hapo Januari 8.

Forum

XS
SM
MD
LG