Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Mei 04, 2024 Local time: 02:42

IMF: Uchumi wa Burundi unatarajiwa kukua kwa asilimia 4.3


Rais wa Burundi Evariste Ndayishimiye alipohutubia kikao cha 77 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Alhamisi, Septemba 22, 2022, kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa. (AP)
Rais wa Burundi Evariste Ndayishimiye alipohutubia kikao cha 77 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Alhamisi, Septemba 22, 2022, kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa. (AP)

Uchumi wa Burundi unatarajiwa kukua kwa asilimia 4.3 mwaka huu kutoka asilimia 2.7 mwaka 2023, ikiwa umesaidiwa na kuboreshwa kwa utendaji katika sekta ya kilimo, Shirika la Kimataifa la Fedha Duniani -IMF lilisema.

Huku ikiwa na idadi ya watu milioni 12, uchumi wa Burundi unategemea kwa kiasi kikubwa katika mapato ya kilimo, haswa kutoka kwenye chai na kahawa.

Ukuaji unatarajiwa kukua kwa haraka ukichangiwa na uzalishaji wenye nguvu katika kilimo, uwekezaji wenye tija, na mageuzi yanayoendelea shirika hilo limesema katika taarifa Jumatatu jioni .

Uhaba wa mafuta ulidumaza harakati za uchumi mwaka 2023, shirika hilo limesema.

Uchumi wa Burundi ndio unaanza kuimarika tena kutokana na mzozo wa miaka mingi na misukosuko ya kisiasa chini ya kiongozi wa zamani Pierre Nkurunziza ambayo iliacha sekta kuu zikiyumba.

Forum

XS
SM
MD
LG