Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 03:11

Burkina Faso yakosolewa vikali kwa kufunga Radio ya Ufaransa ya RFI


Kiongozi wa kijeshi wa Burkina Faso Ibrahim Traore .Oct. 2, 2022.
Kiongozi wa kijeshi wa Burkina Faso Ibrahim Traore .Oct. 2, 2022.

Makundi ya kutetea uhuru wa vyombo vya habari yamekemea hatua ya Burkina Faso ya kusitisha upeperushaji wa habari wa Radio ya  Kimataifa ya Ufarasa ya RFI, ambayo kundi la kijeshi linalotawala limesema inatoa habari zisizo sahihi.

Wakosoaji wanasema kwamba utawala huo unajaribu kudhibiti utaoaji wa habari wakati ukikabiliwa na ukosefu mkubwa wa usalama nchini. Burkina Faso imekuwa taifa la pili baada ya Mali kusitisha utangazaji wa RFI, wakati mataifa yote mawili yakiwa chini ya utawala wa kijeshi.

Muda mfupi baada ya tangazo hilo kufanywa mwishoni mwa wiki, RFI kupitia taarifa ililalamikia hatua hiyo na kusema kwamba ingefanya kila juhudi kuhakikisha kuwa matangazo yake yanarejeshwa.

Taarifa kutoka utawala wa kijeshi wa Burkina Faso ilisema kwamba RFI ilitoa taarifa za kupotosha kuhusiana na madai ya jaribio la mapinduzi wiki iliyopita, na kuwapa sauti wapiganaji wa kiislamu.

XS
SM
MD
LG