Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 01:10

Jimbo la Punjab huko India linapiga kura


Uchaguzi katika jimbo la Punjab nchini India
Uchaguzi katika jimbo la Punjab nchini India

Jimbo la Punjab nchini India linapiga kura katika uchaguzi unaoonekana kama kipimo kwa chama cha Hindu cha Waziri Mkuu Narendra Modi, kabla ya uchaguzi mkuu mwaka 2024.

Chama cha Bharatiya Janata kina matumaini ya kupunguza chuki ya wakulima wa Sikh ambao walipiga kambi kwenye viunga vya New Delhi kwa mwaka mmoja kabla ya Modi kukubali kufuta sheria za mashamba zenye utata.

Wakulima waliogopa sheria zingepunguza mapato yao. Ndio kambi ya upigaji kura yenye ushawishi mkubwa zaidi nchini India, na maandamano yao yanatarajiwa kuwepo katika majimbo mengine manne, ambayo pia yanafanya uchaguzi. Mazingira ya kisiasa yanabadilika na vyama vipya vinajaribu kutafsiri hasira ya wakulima, kuwa kura ya kuzuia BJP kupenya kwenye bakuli la nafaka la India.

XS
SM
MD
LG