Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Februari 11, 2025 Local time: 05:36

Trump asema Tillerson 'apoteza wakati wake'


Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Rex Tillerson, kushoto, akikutana na Kansel wa kitaifa wa China Yang Jiechi kwenye BUnge la Wananchi, Jumamosi, Sept. 30, 2017, mjini Beijing, China.
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Rex Tillerson, kushoto, akikutana na Kansel wa kitaifa wa China Yang Jiechi kwenye BUnge la Wananchi, Jumamosi, Sept. 30, 2017, mjini Beijing, China.

Rais Donald trump wa Marekani amesema Jumapili kwamba amemuambia waziri wake wa mambo ya nchi za nje Rex Tillerson “anapoteza wakati wake kujaribu kujadiliana na kiongozi wa Korea ya Kaskazini.

Katika ujumbe wake wa Twitter amemuambia Rex “usitumiye nguvu zako bure,tutafanya kinachohitajika kufanywa.”

Wachambuzi wanasema haya yanatokana na kwamba siku ya Jumamosi wizara ya mambo ya nje ya Marekani kueleza kwamba Korea ya Ksakazini haijaonesha dalili za kutaka kuanza mazungumzo juu ya mipango yake ya silaha za nuklia na makombora.

Waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani Rex Tillerson, kushoto, akikutana na rais wa China Xi Jinping katika Ukumbi Mkuu wa Wananchi, Jumamosi, Sept. 30, 2017, in Beijing.
Waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani Rex Tillerson, kushoto, akikutana na rais wa China Xi Jinping katika Ukumbi Mkuu wa Wananchi, Jumamosi, Sept. 30, 2017, in Beijing.

Taarifa hiyo inafuatia matamshi ya Tillerson alipokua anakamilisha ziara yake ya Asia mjini Bejing, kukiri kwamba Marekani imekua ikiwasiliana moja kwa moja na Pyongyang.

Waziri huyo alikua China kujaribu kuirai kutumia ushawishi wake kuimwekea shinikizo Kim JOng Un kuacha majaribio yake na kuanza mazungumzo.

XS
SM
MD
LG