Waumini wa Kikristo waandamana kutaka Umoja wa Mataifa usifumbie macho msaada wanaopewa waasi wa M23

Your browser doesn’t support HTML5

Maelfu ya waumini wa Kikristo wameandamana Jumapili kote nchini DRC kulaani ghasia za kivita zinazofanyika mikoa ya mashariki ya nchi hiyo.

Viongozi wa makanisa wahimiza Umoja wa Mataifa kutofumbia macho madai ya kwamba nchi ya Rwanda inawasaidia waasi wa M23 huku wakiomba mauaji yakomeshwe katika maeneo ya mashariki ya nchi hiyo.