Makombora ya Russia yamefyetuliwa hadi mji wa bandari wa Odesa Kusini mwa Ukraine mapema Jumatano, na kuua takriban watu watatu na wengine 13 kujeruhiwa.
Jeshi la Ukraine limesema kwamba makombora yaliyotumiwa katika shambulio hilo ni manne ya kwenda masafa vya mbali yaliyopewa jina la Kalibr.
Maafisa wa jimbo wamesema kuwa makombora yalipiga ghala ambapo watu hao watatu waliuawa na kwamba shambulio la Russia pia liliharibu nyumba na maduka katikati mwa jiji la Odesa.
Maafisa walisema waokoaji walikuwa wakitafuta mtu yeyote ambaye huenda alikuwa amezikwa kwenye vifusi.