Wakosoaji wa Twitter wasema Elon Musk anakurupuka kuongea

Your browser doesn’t support HTML5

Elon Musk amesema Kampuni ya Twitter itaruhusu akaunti za twitter zilizokuwa na tiki ya blue kupiga kura kuhusu mabadiliko ya sera baada ya watumiaji wengi kumpigia kura ya kuachia ngazi kama mkurugenzi mtendaji wa kampuni hiyo.

Musk alizindua kura ya maoni ya twitter wiki iliyopita na asilimia 57.5 ya watumiaji wa mtandao huo alipowauliza iwapo anafaa kujiuzulu kuwa mkurugenzi mtendaji walipiga kura ya ndio. Wakosoaji wa Musk wanaeleza kuwa mara nyingi anaongea kabla ya kutafakari. Endelea kusikiliza sakata hili la Twitter na yale ambayo mkurugenzi huyo anapania kuyatekeleza...