Waislam washerekekea Eid al-Fitr

Waislam wakiswali msikitini Bamako, Mali Agosti 8, 2013.

Waislam duniani kote wanasheherekea sikukuu ya Eid al Fitr Alhamis wakiadhimisha kumalizika kwa mwezi mtukufu wa Ramadhan.

Waumini walikusanyika katika misikiti huko Indonesia nchi yenye waislam wengi kuliko zote duniani kwa sikukuu hiyo ya Eid leo.

Sherehe za Eid pia ziliadhimishwa Saudi Arabia, Syria na Malaysia.
Nchini Misri, makundi ya waumini waliomba na kusheherekea katika uwanja wa Tahrir Square, wakati viongozi wa muda wa Misri wakihudhuria sala ya Eid katika mji huo mkuu.

Waislam huko Kenya na Tanzania wanasherehekea siku kuu hiyo ya Eid al-Fitr kesho Ijumaa