Rais wa Ufaransa Francois Hollande, amesema Waislam wa kawaida ndio waathirika wa mwanzo wa Uislam wenye msimamo mkali.
Rais Hollande alizungumza hayo katika Taasisi ya Arab World, mjini Paris, Ufaransa, ambapo taasisi hiyo inafanya juhudi za kuleta uhusiano baina ya Ufaransa na tamaduni za kiarabu.
Ufaransa inaendelea kushughulika na mashambulizi ya kigaidi ya wiki iliyopita yaliyofanywa na waislam wenye msimamo mkali waliokuwa na uhusiano na Al-Qaida.
Amesema kadhia kama ya wiki iliyopita ya mashambulizi katika jarida la Charlie Hebdo, inaweza kutumika kuondoa hali ya kuaminiana ama kufanya watu kutoa ujumbe wao kwa kutumia “vitendo vibaya zaidi.”