Waandamanaji washutumu utawala wa Netanyahu ni wakibaguzi

Your browser doesn’t support HTML5

Maelfu ya watu wameandamana nje ya bunge la Israel, wakati baraza la mawaziri lililoteuliwa na waziri mkuu wa nchi hiyo Benjamin Netanyahu linaapishwa.

Netanyahu anatarajiwa kurudi madarakani akiapa kutekeleza sera ambazo zinaweza kusababisha mgogoro ndani na nje ya Israel, na kupelekea Israel kutengwa na washirika wake wa karibu.

Viongozi wa upinzani wa Israel wameeleza kupinga kabisa msimamo wa Netanyahu wakati anatarajia kutangaza sera zake kwa taifa.Serikali mpya imeapishwa hii leo. Waandamanaji waliopeperusha bendera wamepaaza sauti wakishutumu utawala wa Netanyahu kwa ubaguzi.