Mkutano huo pia utajadili suala la kutolewa fedha zaidi kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa pamoja na kuanza mpango wa mfumo mpya wa fedha duniani.
Mkutano huo wa ngazi ya juu wa siku mbili unawaleta pamoja karibu viongozi 50 katika mji mkuu wa Ufaransa, Paris ili kujaribu kufikia maridhiano juu ya namna ya kuendelea mbele na baadhi ya mipango ya kimataifa ambayo inasuasua inayosimamiwa na mashirika makuu kama Umoja wa Mataifa, Benki Kuu ya Dunia na G20.