UN yatahadharisha kuzuka njaa na vifo Tigray

Your browser doesn’t support HTML5

Hali ya njaa inakadiriwa itatokea katika eneo lenye vita la kaskazini, na maelfu ya watu inawezekana wakafariki – hivyo ndivyo Umoja wa Mataifa (UN) inaelezea hali ya huko Tigray.
Kwa wagonjwa wengi kwenye hospitali ya rufaa katika mji mkuu wa Mekele, huu ndio mwisho wa safari ndefu na ngumu.

Wameliambia Shirika la Habari la Associated Press jinsi wanajeshi wa Ethiopia na Eriteria walivyoiba chakula chao na kuteketeza mashamba yao.

Huku hospitali za karibu zikiwa zimeibiwa vifaa au kuharibiwa, hawana sehemu nyingine ya kwenda. Na madaktari wanasema kuwa hili ni sehemu ya tatizo kubwa zaidi.