Ujumbe wa Rais Biden kwa viongozi wa Umoja wa Afrika

Your browser doesn’t support HTML5

Uongozi wa Rais Joe Biden na Makamu Rais Kamala Harris umeahidi kushirikiana na Umoja wa Afrika ili kufikia azma yao ya pamoja ya mustakbali uliokuwa bora wakati Biden akihutubia mkutano wa viongozi wa umoja huo kwa njia ya mawasiliano ya mtandao.
Biden akitanguliza ujumbe huo kabla ya mkutano wa 34 wa marais na viongozi wa Umoja wa Afrika Mwaka 2021 amesema utawala wake uko tayari kujenga tena ushirikiano duniani na kujihusisha tena na taasisi za kimataifa kama vile Umoja wa Afrika.