Taharuki mjini Goma baada ya Volcano kulipuka

Your browser doesn’t support HTML5

Gavana wa jimbo la Kivu Kaskazini Jenerali Constant Ndima amesema wakati hayo yakijiri mjini Goma, matope ya moto ambayo yamekuwa yakiteremka katika mlima huo baada ya kulipuka kwa Volcano ya mlima Nyiragongo na kuishia nje kidogo ya mji Goma.

Kiongozi huyo amesema tathmini ya awali inaonyesha watu watano wamefariki hadi sasa.

Kulingana na Shirika la Habari la AFP watu wamerejea kwenye makazi yao mchana huu baada hatari hiyo ya matope ya moto kupungua kwa kiasi fulani.