Polisi wafunga eneo lote la Bunge la Marekani Ijumaa

Your browser doesn’t support HTML5

Polisi walifunga majengo ya Bunge la Marekani Ijumaa mchana baada ya kuripotiwa milio ya risasi katika eneo hilo.
Katika tukio hilo afisa mmoja wa polisi wa Bunge la Marekani ameuawa na mwengine amejeruhiwa Ijumaa wakati dereva mmoja alipoliingiza gari kugonga kizuizi nje ya Bunge la Marekani.

Polisi Bungeni wamesema mshukiwa huyo aliteremka na kisu mkononi na kuelekea kuwashambulia maafisa wa polisi. Polisi hao walimrushia risasi mtu huyo. Mshukiwa huyo ametambuliwa kwa majina ya Noah Green na ana umri wa miaka 25. Polisi wanafanya uchunguzi wa historia yake kupata fununu kilichomsukuma kufanya shambuliz hilo.